AS Roma
imeshinda michezo mitano
kati ya sita
ya mwisho katika ‘Derby della Capitale’ dhidi
ya mahasimu wao
wa jiji ‘Takatifu’ la Roma, SS Lazio. Michezo sita
ya mwisho kati
ya timu hizo
ilikuwa katika Serie
A na Lazio wamefanikiwa
kuambulia sare moja
tu, Januari 11, 2015
walipofungana 2-2.
Timu hizo zinakutana
tena usiku wa
Jumatano hii katika mchezo
wa nusu fainali
ya kwanza michuano ya
Coppa Italia huku
Lazio wakiwa wenyeji katika uwanja
wa Estadio Olimpico. Lazio imepoteza
michezo yote mitatu
ya mwisho baina
yao ambayo walikuwa
wenyeji huku kipigo cha
mwisho wakipata Desemba 4, 2016
kwa kulazwa 2-0.
Simone Inzaghi (kaka
wa Phillipo Inzaghi) aliiongoza timu yake kuwatoa
Inter Milan katika
hatua ya robo
fainali mwezi uliopita
anamtegemea zaidi mshambulizi, Ciro Immobile, kiungo Muargentina Lucas Bilglia huku kikosi
chake kikiwa kimeshinda michezo minne na
kupata sare moja
katika game tano
za mwisho katika
michuano yote.
Luciano Spalletti ambaye
timu yake iliitoa
Cecena katika robo
fainali anaweza kumuanzisha mkongwe
Francisco Totti na Stephan El
Shaarawy ambao wamekuwa wakitumika
zaidi katika michuano
hiyo lakini pia
anaweza kubadili uamuzi
na kupanga safu
yake hatari ya
mashambulizi ambayo imefunga magoli
11 katika michezo
minne iliyopita.
Edin Dzeko anaweza
kusimama kama mshambulizi
pekee, huku katikati
wakipangwa viungo watano Mohamed Salah, nahodha Daniele De
Rossi, Kevin Strootman, Bruno
Perez na Radja
Nainggolan ambao walianza katika
mchezo wa ushindi
wa 3-1 ugenini
dhidi ya Inter
Milan katika ligi
kuu Jumapili iliyopita.
Mechi ya Lazio
dhidi ya Roma
ni kati ya
michezo mitano bora
ya ‘wapinzani wa jadi’
duniani huku mipambano
yao ikizusha vurugu
za mara kwa
mara ndani na
nje ya uwanja.
No comments:
Post a Comment