TANGAZA NASI HAPA

Wednesday, 8 March 2017

UEFA CL: Barcelona yapindua matokeo na kufuzu robo fainali…..




BARCELONA imekuwa timu ya kwanza barani ulaya kupindua matokeo ya 4-0 na kufuzu kwa hatua inayofuata ya michuano ya ligi ya mabingwa.
Magoli matatu ndani ya dakika tatu za mwisho  kutoka kwa Neymar Jr dakika za 88’ na 90’ alilofunga kwanjia ya penalty na lile la mwisho kutoka kwa Sergi Roberto  yameipeleka Barca robo fainali baada ya kushinda 6-1 usiku wa Jumatano na kufuzu kwa matokeo ya jumla 6-5 dhidi ya PSG. Neymar alitajwa kuwa mchezaji bora wa mechi hiyo.
Luis Suarez alifunga goli la kuongoza  dakika ya 3’ tu ya mchezo,mlinzi Layvin Kurzawa akajifunga dakika ya 40’ na kufanya mchezo kwenda mapumziko Barcelona wakiongoza 2-0. Kocha Luis Enrique  alibadilisha mfumo wa kiuchezaji ambao ulimfanya Lionel Messi kucheza eneo la kiungo.

Enrique  aliwapanga walinzi watatu nyuma,Samuel Umtiti, Javier Madcherano na Gerlad Pique. Katika kiungo akawapanga Messi,nahodha Andres Iniesta, Sergio Busquets na Ivan Rakitic huku washambuliaji wakiwapangwa Rafihna Alcantara, Suarez na Neymar.
Messi alifunga goli la tatu kwa mkwaju wa penalty dakika ya 50’ . mshambulizi Edson Cavanni alifunga alimalizia pasi ya Kurzawa dakika ya 62 na kuwafungia Waparis hao goli muhimu la ugenini na bao hilo lilimaanisha Barca inapaswa kushinda kuanzia 6-1.

Dakika zikiwa zimeyoyoma Neymar akafunga mara mbili kasha Roberto akamalizia goli muhimu zaidi dakika ya mwisho akimalizia pasi ya Neymar na kuifanya Barca kushinda 6-1  na kuwatupa nje mabingwa hao wa Ligue 1.

No comments:

Post a Comment