TANGAZA NASI HAPA

Wednesday, 1 March 2017

VPL: Msuva apiga goli la 12, Yanga pungufu mchezaji mmoja ikiichapa Shooting…




 WAKICHEZA pungufu  mchezaji  mmoja  kwa  zaidi  ya  dakika  45, mabingwa  watetezi  wa  ligi  kuu  Tanzania  Bara, Yanga  SC  wamefanikiwa  kushinda 2-0  dhidi  ya  Ruvu  Shooting katika  mchezo  uliopigwa  uwanja  wa  Taifa  Dar  es  Salaam  jioni hii huku  mlinzi  wa  kati  raia  wa  Togo, Vicent  Bossou  akicheza  kwa  kiwango  kizuri.

Mshambulizi  raia  wa  Zambia  Obrey  Chirwa  alioneshwa  kadi  ya  njano  dakika  ya  44 kwa  kosa la kufunga goli kwa mkono na kumsukuma  golikipa  wa  Shooting, Bidii  Hussein   na  dakika  moja  baadae  akapewa ya pili ya  njano iliyoambatana na  kadi  nyekundu na  mwamuzi, Ahmada Simba kwa  kosa  la  kuutupa  mpira  chini  kwa  hasira na kuwaacha  pungufu  wenzake.
 Kiungo mshambulizi, Saimon  Msuva  alifunga  goli  lake  la  12  msimu  huu  kwa  njia  ya  mkwaju  wa  penalty  dakika  ya  32. Goli  hilo  lilidumu hadi  kipindi  cha  kwanza  kinamalizika. Mtokea  benchi, Emmanuel  Martin  akaongeza  goli  la  pili  dakika  ya  90’. Martin  aliingia  dakika 12  kabla  ya  kumalizika  kwa  mchezo  akichukua  nafasi  ya Deus  Kaseke. 
 Kwa matokeo  hayo  Yanga  imefikisha  pointi 52  baada  ya  kucheza  michezo  23 (pointi  mbili  nyuma  ya  vinara Simba  SC) Mwishoni  mwa  wiki  hii  kikosi  cha  kocha  George  Lwandamina  kitaivaa  Mtibwa  Sugar  katika  uwanja  wa  Jamhuri, Morogoro  wakati  Simba  watacheza  na  Mbeya  City  FC  katika uwanja  wa  Taifa.

No comments:

Post a Comment