Na Baraka Mbolembole
Msuva
amekuwa akikosolewa sana na mashabiki wa klabu yake. Si yeye tu, Mnyarwanda,
Haruna Niyonzima, na sasa mashabiki wa Yanga wamehamia hadi kwa mlinzi wa kati
Mtogo, Vicent Bossou na mshambulizi Mzimbabwe, Donald Ngoma.
Chanzo
cha mashabiki wa Yanga kumzomea mara kwa mara Msuva na kumkosoa Niyonzima ni
kwasababu 'wanaamini' wachezaji hao 'wana mapenzi na mahasimu wao Simba SC.
Msuva ni mchezaji mwenye kipaji kikubwa
miongoni mwa wachezaji wa Yanga, ana akili sana pindi unapomweleza jambo ndio
maana ninaamini baadhi ya mashabiki wa klabu yake wanakosea sana wanapomtuhumu
mchezaji ambaye alifunga magoli 17 na kushinda tuzo binafsi ya mfungaji bora
katika ligi kuu Tanzania bara misimu miwili iliyopita.
Wanakosea zaidi wanamtuhumu kucheza chini ya kiwango wakati tayari amehusika
kikamilifu katika magoli zaidi ya 20 ya timu katika ligi inayoendelea hivi
sasa. Tangu alipoingia katika timu hiyo akiwa kinda wa U19 mwaka 2012 hadi sasa
akiwa na miaka 23 bila shaka kiungo huyo mshambulizi wa pembeni amefanya
jitihada kubwa na ataendelea kufanya vizuri kutokana na utulivu wake.
Kama mchezaji aliyeingia Yanga akiwa
hana uzoefu, Msuva amesimamiwa na makocha, Tom Saintfiet raia wa Ubelgiji,
Waholland, Ernie Brandts na Hans van der Pluijm, raia wa Brazil, Marcio Maximo
na sasa anaendelea kukua vizuri kimchezo chini ya Mzambia, George Lwandamina.
Naamini kama mwanadamu amelinda 'utu'
wake, hana ubinafsi na amekuwa akicheza kitimu ili kupata mafanikio ndiyo maana
katika misimu yake mitano klabuni hapo amefunga zaidi ya magoli 60, ameisaidia
klabu kushinda mataji matatu ya ligi kuu (2012/13, 2014/15, na 2015/16)
Amekuwa mstali wa mbele kupigania taji
la tatu mfululizo la klabu, amesaidia mataji mawili ya Ngao ya Jamii na moja la
michuano ya FA Cup, pia alikuwa ni sehemu ya wachezaji muhimu walioisaidia
Yanga kufuzu kwa mara ya kwanza katika hatua ya makuodi ya Caf Confederation Cup
2016.
Msuva amekuwa katika kiwango bora
kabisa kwa misimu mitatu sasa, na anaweza kufikia mafanikio makubwa zaidi kama
mashabiki wa klabu yake wataendelea kuwa upande wake japokuwa mashabiki ni
'watu wanaopenda kupita kiasi' hivyo wanataraji mambo mazuri tu kila wakati.
Mtibwa Sugar siku ya jana Jumapili.
Nimemsikia akisema alipaisha penalti ile
kutokana na 'imani ya kishirikina' siamini kama ni kweli
kwa sababu ile tayari alikwishapoteza penalti mbili ndani ya miezi mitatu ya
mwaka huu. Inawezekana hakuna mchezaji mwingine anayejiamini katika upigaji wa
mikwaju ya penalti katika tinu ya Yanga kama Msuva ndiyo maana amekuwa
akiendelea kubeba majukumu hayo licha ya kupoteza mara kwa mara.
Yanga kama timu imekosa kujiamini
katika upigaji wa mikwaju ya penalti kwa miaka zaidi ya miwili sasa. Na kwa
timu inayocheza mara kwa mara katika michuano ya 'mtoano' inaonesha wazi
hawafanyi mazoezi ya kutosha katika eneo hilo.
Baada ya kupoteza mkwaju wa penalti
siku ya jana wengi wa mashabiki wa Yanga wanahoji ni
kwanini Nahodha, Nadir hakukwenda kupiga au Kelvin Yondan? Upande wangu nadhani
hilo ni tatizo la timu nzima ndiyo maana katika miaka ya karibuni magolikipa,
Ally Mustapha na Deo Dida wamekuwa wakijibebesha majukumu hayo lakini nao
tumeshuhudia wakipoteza mara kadhaa.
inayofuatiliwa sana.
No comments:
Post a Comment