TANGAZA NASI HAPA

Monday, 13 March 2017

Jicho la 3; Yanga 1-1 Zanaco, tatizo ni Lwandamina na mbinu zake mbovu, kutoamini vipaji vingine…





Na Baraka Mbolembole


HATA kabla ya mabadiliko ya kutoka na kuingia Deus Kaseke dakika za mwisho tayari ‘nilishang’amua’ uwezo mdogo wa kocha George Lwandamina.

Mkufunzi huyo mkuu wa Yanga SC raia wa Zamabia sasa  atahitaji kufanya ‘ushawishi’ mkubwa kwa mashabiki wa timu hiyo ili kumuamini kuwa ni ‘kocha sahihi’ wa kuisogeza mbele timu bora iliyoachwa na mtangulizi wake Mholland,Hans van der Pluijm.

Kila mtazamaji wa mchezo wa Jumamosi hiii kati ya wenyeji Yanga dhidi ya Zanaco FC kutoka Zambia alifurahishwa na uwezo wa juu ulioneshwa na  kiungo mchezesha timu wa Zanaco, Zimbseleni Moyo ambaye alitawala kiungo katika mchezo huo wa kwanza  hatua ya mwisho ya mtoano kuwania kufuzu kwa makundi.

Kila ‘Mzalendo’ alitaraji matokeo bora kwa wawakilishi hao wa Tanzania Bara,lakini wengi waliishia kulaumu kiwango cha timu ndani ya uwanja na timu ya ushindi. Siku mbili kabla ya mechi niliandika kwamba  kocha wa Yanga, Lwandamina na wasaidizi wanapaswa kuundaa ‘timu mpya ya mpito’ kutokana na wachezaji wengi muhimu kuwa na majeraha.

Licha ya ‘kulazimishwa kucheza’ huku wakiwa na maumivu  Wazimbabwe, Donald Ngoma na Thaban Kamusoko kikosi cha Yanga kilionekana kitakabaliwa na ‘mchezo mgumu’ katika uwanja wa nyumbani mbele ya mabingwa hao wa Zambia, huku habari za wachezaji kupoteza morali kutokana na ukosefu wa mishahara zikiongeza wasiwasi kama kweli timu iko tayari kwa mchezo huo muhimu.

Presha bila shaka ilikuwa kubwa kwa Lwandamina,huku kuwakosa wachezaji wake Amis Tambwe,Haruna Niyonzima kukimaanisha timu ‘itakosa makali’ katika ushambuliaji na ufungaji.

Bila Ngoma aliye katika makali, Yanga ilianza mchezo ikiwa na mshambulizi mmoja, viungo wawawili wa pembeni ( Saimon Msuva na Obrey Chirwa,) na viungo watatu katikati ya uwanja ( Kelvin Yondan, Justine Zulu na Thaban.) Hassan Kessy na Mwinyi Hajji katika beki za pembeni,nahodha Kelvin Yondan na Vicent Bossou katika ulinzi wa kati.

Katika benchi walikuwepo golikipa Ally Mustapha, walinzi watatu Oscar Joshua, Juma Abdul, na Vicent Andrew, pia walikuwepo viungo watatu wa mashambulizi, Deus Kaseke, Juma Mahadhi na Emmanuel Martin ambao wote walipata nafasi ya kucheza kipindi cha pili.

Katika muda wote wa dakika 60’ alizokuwa uwanjani,Ngoma alikuwa ‘mtu wa mashabiki’ wa Yanga na ‘hakubanduka midomoni mwao’ hata pale alipotolewa na nafasi yake kuchukuliwa na Mahadhi. Ngoma alionekana ‘kupwaya’ katika  mfumo ambao ulimfanya acheze kama mshambulizi pekee, huku Kamusoko akicheza nyuma yake.

Alipokuwa akigusa mpira alionekana hayupo ‘fiti’na nafikiri hata kocha Lwandamina alikosea kumpanga mshambulizi huyo pekee. Kwa kutambua majeraha aliyonayo,Lwandamina alipaswa kumpanga Ngoma sambamba na Chirwa katika mfumo wa 4-4-2 ili kumsaidia mchezaji huyo ‘aliyejitolea kuccheza japokuwa hayupo tayari kimwili.’

Ndiyo,Ngoma alionresha kiwango cha kufadhaisha sana lakini uwepo wake uwanjani uliisaidia Yanga kuwa salama kwa sababu wachezaji wa Zanaco wanafahamu kuhusu makali yake katika ufungaji. Hivyo hawakusogea kwenda mbele.

Upande wangu nitaendelea kumlaumu kocha Lwandamina kwa sababu hakujiandaa kukabiliana na majeraha  yanayoisumbua timu yake,na ni yeye ndiye sababu ya kiwango kibovu cha timu. Wachezaji wengi wamekuwa wakilalamikia nafasi wanazochezeshwa na kocha huyo,jambo ambalo limefanya washindwe kutoa matokeo mazuri kama ilivyokuwa wakati wa Hans van der Pluijm.

Mfumo wa kumpanga Ngoma pekee wakati akiwa na majeraha uliimaliza timu ndiyo maana mpira haukuwa ukikaa mbele walau kwa dakika moja tu. Ndiyo wachezaji wanaweza kufanya vyema katika mfumo wowote, lakini si rahisi ikiwa hawapo ‘fit’ kimwili na kiakili. Ngoma amecheza mara kadhaa kama mshambulizi ‘huru’ wakati wa Hans na alifanya vizuri kwa sababu alicheza akiwa bila maumivu.

Bahati mbaya kwa Lwandamina ni kwamba Ngoma na Kamusoko walicheza pasipo kujiamini na wakati mechi ikiendelea wakaonekana hadi na wapinzani wao kwamba hawako ‘fit’ Lwandamina alianza kupunguza makali ya timu kutokana na mfumo wake na kutowaamini vijana wenye vipaji kama Hassan Mhilu ambaye angeweza kufanya vizuri zaidi ya Kelvin Yondan ambaye alichezeshwa namba sita.

Baada ya kipigo cha 4-0 kutoka kwa Azam FC katika michuano ya Mapinduzi Cupmapema mwezi Januari nilianza kujenga hofu kuhusu mbinu za Lwandamina,mechi mbili alizoisimamia Yanga vs Simba ( Mapinduzi Cup na ligi kuu,) na baadaye suluhu-tasa dhidi ya Mtibwa sikuwana shaka tena zaidi ya kuamini chini ya Mzambia huyu Yanga itapata wakati mgumu.

Sasa timu ambayo ilikuwa katika kiwango cha juu kiuchezaji,hamasa,uwajibikaji imebadilika huku wachezaji wakiendelea kushuka viwango kila leo. Kama wachezaji wanashuka viwango hii inamaanisha kuwa uwezo wa kocha nimdogo.

Upande wangu ni mmoja kati ya wanaohitajimatokeo bora,kocha kama huna uwezo wa kupanga kikosi na kufanya mabadiliko basi ‘hukidhi’mahitaji ya timu. Lwandamina alipaswa kumuanzisha Deus Kaseke au Mhilu katika wing mojawapo sambamba na Saimon Msuva huku Ngoma na Chirwa wakicheza kama washambuliaji ‘wanaotegemeana.’

Unapokutana na timu iliyo bora katika kiungo,kama ilivyokuwa kwa Zanaco alafu unamtoa mchezaji kama Kamusoko ambaye alikuwa bora kuliko wote upande wako na kumuingiza Mahadhi ambaye hana uwezo mkubwa wa kukaa katikati ya uwanja, ni dalili za kuwafanya watu waendelee kuhoji kuhusu uwezo wa Lwandamina.

Inakuwaje aliingiza timu yake katika mfumo wa kuzuia katika uwanja wa nyumbani? Lwandamina hakupaswa kujaribu mfumo katika mechi muhimu,na alipaswa kumuweka benchi Kelvin au ili kutoa nafasi kwa wachezaji asilia wa nafasi ya kiungo kuchukua mipira nyuma na kuipeleka mbele jambo ambalo Kelvin alishindwa na matokeo yake mipira ikawa inapigwa kutoka nyuma kwenda mbele bila mpangilio wa mashambulizi.

Kiwango cha chini walichoonesha Yanga katika mchezo wa kwanza kimezua wasiwasi kama kwelitimu hiyo itaweza kusonga mbele ikicheza ugenini. Walizuia vibaya,walipanga mashambulizi vibaya,na hawakuwana ubora katika mashambulizi.

No comments:

Post a Comment