TANGAZA NASI HAPA

Thursday, 9 March 2017

Emery; Kufungwa 6-1 ‘ni siku mbaya’ kwa Paris…




BAADA ya kupoteza uongozi wa 4-0 walioupata katika mchezo wa kwanza jijini Paris kocha wa Paris St.German, Unal Emery amesema kipigo cha 6-1 walichokumbana nacho Nou Camp kutoka kwa FC Barcelona kimemuumiza kila mmoja katika klabu yake.

Paris imeondolewa kwa jumla ya magoli 6-5 na kushindwa kwa mara ya tatu kuwaondoa Barcelona katika michuano ya mabingwa ulaya usiku wa Jumatano hii. 

Magoli matatu ndani ya dakika tatu za mwisho yaliyofungwa na Neymar Jr aliyefunga mawili dakika za 88’ na 90’na lile la Sergio Roberto dakika ya mwisho ya mchezo yamewaumiza mmno wapenzi wa timu hiyo ya Ufaransa.

“Kwa kila mmoja ndani ya Paris Saint-Germain, viongozi, wachezaji pamoja na mashabiki hii ilikuwa ni siku mbaya kwao. Kilichotokea uwanjani ni kitu ambacho hakuwahi kukipitia,” alisema Emery.

“Tumepoteza nafasi nzuri ya kusonga mbele. Tulitaka kukua kulingana na mchezo, kipindi cha kwanza hatukucheza kwa kiwango tulichotaka. Tulitaka kucheza kama mchezo wa kwanza, tulitaka kucheza mtindo wa counter-attack. Baada ya goli la tatu timu ilikuwa vizuri, tulihitaji kupata matokeo mazuri kwa kufunga goli la pili.”

“Ndani ya dakika tano, tulipoteza kila kitu. Hatukuwa na uwezo wa kujilinda. Ni experience mbaya kwetu, lakini ni somo. Najifunza kupitia kushindwa, ni wazi tumepoteza fursa nzuri.”


No comments:

Post a Comment