TANGAZA NASI HAPA

Thursday, 9 March 2017

Mwambusi: Tambwe, Ngoma wana asilimia 50 tu ya kuwavaa Zanaco, lakini…..



 
Kuelekea mchezo wa ligi ya mabingwa Afrika siku ya kesho katu ya wenyeji Yanga SC vs Zanaco FC ya Zambia kocha msaidizi wa mabingwa hao wa Tanzania Bara,Juma Mwambusi amesema kuna asilimia 50 tu za kuwatumia washambuliaji wao wa kigeni Mzimbabwe, Donald Ngoma na Mrundi, Amis Tambwe.

Washambuliaji hao wawili wamekuwa wakisumbuliwa na maumivu. Ngoma amekuwa akisumbuliwa na maumivu ya goti sawa na Tambwe, lakini kuna uhakika wa kiungoMzimbabwe Thaban Kamusoko kucheza mchezo huo muhimu kwa wawakilishi hao wa Bara.

“ Tunakwenda kucheza mechi ngumu ya hatua ya mtoano, tunacheza nyumbani. Tunashukuru maandalizi yanakwenda vizuri hadi sasa pamoja na uwepowa majeruhi na wachezaji  waliokuwa na majeraha. Kikubwa kuna wachezaji ambao kila siku walikuwa wakifanya mazoezi vizuri, wako tayari kwa mchezo.”

“ Kwa wale wachezaji waliokuwa na majeraha kwa muda mrefu tunaendelea kutazama maendeleo yao,bado kuna siku moja ya kuendelea kujilidhisha kuhusu utayari wao wa kushirikimchezowa Jumamosi, vinginevyo Yanga ina kikosi kipana,kwa hiyo wachezaji wengine waliopo wanaweza kutuwakilisha vizuri katika mchezo wetu.”

“ Tumeshacheza michezo mingi bila ya wachezaji waliokuwa na majeraha  na tukapata matokeo, hivyo ieleweke kabisa wachezaji waliosajiliwa Yanga wote  wanaweza kuitumikia timu vizuri. Tumeona Ngoma amerudi lakini hatujajua kama anaweza kucheza, Tambwe alikuwa najeraha la mguu lakini ameanza mazoezi kwa hiyo naweza kusema wachezaji hawa wako na asilimia 50 kwa 50 kucheza mchezo ujao lakini Kamusoko atakuwa tayari kucheza kwa sababu maumivu yake yamepungua kwa kiasi kikubwa.”




No comments:

Post a Comment