TANGAZA NASI HAPA

Friday, 3 March 2017

Hajji Manara, Musa Mgosi wameonekana ARC Hotel Morogoro na baadhi ya wachezaji wa Mtibwa jioni hii




 WAKATI Simba SC ikitaraji kucheza na Mbeya City FC siku ya kesho Jumamosi katika uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, msemaji wa timu hiyo Hajji Manara na meneja wa timu Musa Hassan Mgosi jioni hii ( leo Ijumaa) wameonekana ARC Hotel iliyopo Morogoro pamoja na baadhi ya wachezaji wa Mtibwa Sugar.

Mtibwa itacheza na Yanga SC siku ya Jumapili katika muendelezo wa michezo ya ligi kuu na kuna uwezekano viongozi hao wa Simba ‘wamekwenda’ kuweka 'hasama' ili timu hiyo iisimamishe Yanga ambao wanakimbizana na Simba katika mbio za ubingwa wa ligi kuu msimu huu.

Simba wanaongoza ligi hiyo kwa tofauti ya pointi mbili mbele ya Yanga huku kila timu ikiwa imeshacheza jumla ya michezo 23.

No comments:

Post a Comment