TANGAZA NASI HAPA

Sunday, 5 March 2017

VPL: Yanga SC 'yakwama' kwenda kileleni...





MABINGWA watetezi wa ligi kuu Tanzania Bara, Yanga SC imeshindwa kurejea kileleni mwa msimamo baada ya kulazimishwa suluhu-tasa dhidi ya Mtibwa Sugar katika mchezo uliopigwa uwanja wa Jamhuri, Morogoro jioni hii.

 Kiungo-mshmbulizi, Saimon Msuva alipaisha mkwaju wa penalti dakika ya 35' katika mchezo huo. Yanga walipata penalti hiyo kufuatia mlinzi wa Mtibwa, Lundenga 'kuunawa' mpira akiwa ndani ya eneo la hatari wakati akijaribu kuzuia mpira uliopigwa na mshambulizi wa Yanga, Mzambia, Obrey Chirwa.

 Kwa matokeo hayo Yanga wameendelea kubaki nafasi ya pili wakiwa na pointi 53, alama mbili nyuma ya vinara Simba huku zikiwa zimesalia mechi sita tu kabla ya kumalizika kwa msimu.

No comments:

Post a Comment