Geofrey Mwashuiya alifunga goli la uongozi
dakika ya 13' kisha Chirwa akafunga goli lake la kwanza. Edgar Charles alifunga
goli la kufutia machoni upande wa Kiluvya dakika ya 41'. Dakika tano baada ya
Chirwa kukamilisha 'hat trick' yake, kiungo mshambulizi Juma Mahadhi akafunga
goli la tano dakika ya 75'.
Mabingwa hao watetezi wa michuano hiyo sasa
wamefuzu kwa robo fainali na kuungana na timu za Mbao FC ya Mwanza, Madini FC
ya Arusha, Simba SC na Azam FC za Dar es Salaam, Ndanda FC ya Mtwara na
Tanzania Prisons ya Mbeya.
No comments:
Post a Comment