TANGAZA NASI HAPA

Saturday, 4 March 2017

VPL: ‘Tuta’ lawanusuru Simba SC mbele ya Mbeya City FC







GOLI la mkwaju wa penalty lililofungwa na kiungo-mshambulizi, Shiza Kichuya dakika nne kabla ya kumalizika kwa  mchezo limeinusuru Simba SC kuambulia kichapo mbele ya Mbeya City FC katika mchezo wa ligi kuu Tanzania Bara uliopigwa katika uwanja wa Taifa Dar es Salaam jioni hii.


Ditram Nchimbi ambaye alikuwa katika ubora wa juu licha ya kupoteza nafasi kadhaa  za wazi alifunga goli la uongozi upande wa Mbeya City dakika ya 37’ baada ya kupiga kiki kali iliyombabatiza mlinzi wa Ahmad Juma na kutinga wavuzi. Nchimbi alipokea pasi maridadi ya kisigino iliyopigwa na kiungo mshambulizi, Raphael  kabla ya kufunga.

Mshambulizi, Ibrahim Ajib aliisawazishia Simba dakika ya 65’ kwa mkwaju wa faulo kufuatia kiungo Mohamed Ibrahim kuangushwa karibu na eneo  la mita 18.
Pasi za ‘One-Two’ kati ya nahodha wa City, Kenny Ally na Raphael Breyson , kasha Nchimbi kupiga pasi maridadi ya mwisho ilizaa goli la pili dakika ya 78’ mfungaji akiwa Kenny. Nchimbi angeweza kufunga goli la tatu dakika ya 85’ baada ya kubaki yeye na kipa Daniel Agyei lakini umakini mdogo ukamnyima nafasi ya kufunga.
Baada ya kukoswa goli la tatu Simba walifanya shambulizi la kustukiza ambalo lilizaa mkwaju wa penalty kufuatia kuangushwa ndani ya eneo la hatari kwa mlinzi wa pembeni Mohamed Hussein ‘Zimbwe Jr’ dakika ya 86’ na Kichuya akaukwamisha mpira nyavuni na kufikisha goli lake la 11  msimu huu. Penalti hiyo ililalamikiwa sana na wachezaji wa City.
Kutokana na matokeo hayo Simba imeendelea kubaki kileleni mwa msimamo huku wakiwa na alama 55, ikiwa Yanga wataishinda Mtibwa siku ya kesho watapanda juu ya msimamo kutokana na wastani wao mzuri wa magoli ya kufunga na kufungwa.

No comments:

Post a Comment