TANGAZA NASI HAPA

Friday, 3 March 2017

BUNDESLIGA: RasenBallsport Leipzig yaangusha pointi, Dortimund v Leverkusen uwanjani leo




IKICHEZA ugenini WWK Arena ‘wabishi’ RasenBallsport Leipzig wamevutwa shati baada ya kulazimishwa sare ya kufunganga 2-2 na Augsburg  mchezo uliopigwa usiku wa Ijumaa.

Konstantinos Stafylidis aliwafungia wenyeji goli la uongozi dakika ya 19’,lakini goli hilo lilidumu kwa dakika sita tu kabla ya kusawazishwa na mshambulizi, Timo Werne. Timuhizo zilikwenda mapumziko zkiwa sare ya kufungana 1-1.

 Marvin Compper akaongeza goli la pili upande wa wageni dakika ya 52’, kabla ya Martin Hinteregger kusawazisha dakika ya 60 na kufanya mchezo huo kumalizika kwa sare ya kufungana 2-2.

Ligi hiyo ya Ujerumani itaendelea leo Jumamosi kwa michezo sita kupigwa katika viwanja tofauti huku mchezo kati ya Borussia Dortimund na Bayer Leverkusen katika uwanja wa Iduna Park ukitaraji kutazamwa na wengi.

Ratiba kamili ya mechi za leo ni kama ifuatavyo

16:30 Borussia Dortmund ? - ?  Bayer Leverkusen

16:30 FC Cologne ? - ?  Bayern Munich

16:30 Hoffenheim ? - ?  Ingolstadt

16:30 Mainz 05 ? - ?  Wolfsburg

16:30 Werder Bremen ? - ?  Darmstadt

19:30 Borussia Moenchengladbach ? - ?  Schalke 04


No comments:

Post a Comment