TANGAZA NASI HAPA

Thursday, 9 March 2017

Samata ‘apiga mbili’ KRC Genk ikikaribia kufuzu robo fainali Europa league




MSHAMBULIZI na nahodha wa timu ya Taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars,Mbwana Samata usiku wa Alhamis alifanikiwa kufunga magoli mawili na kuisaidia timu yake ya KRC Genk kuifunga KAA Gent 5-2 katika mchezo wa kwanza ugenini hatua ya 16 bora katika michuano ya Europa League.
Malinovsky alianza kuifungia Genk goli la kwanza kwa shuti la mpira faulo  nje kidogo ya eneo la hatari,  wenyeji wakasawazisha goli hilo kupitia kwa Samuel Kalu dakika ya 27.
 Dakika ya 33 Omary Colley akaifungia Genk bao la pili akiunganisha kwa kichwa mpira wa kona uliopigwa kwa mguu wa kushoto na  Malinovsky. Dakika nne kabla ya mapumziko Samata akafunga akiwa ndani ya eneo la hatari, ksha Jere Uronen  akafunga la nne dakika ya mwisho ya kipindi cha kwanza na  kuifanya Genk kwenda mapumziko wakiwa mbele kwa mabao 4-1.
Dakika 16 kabla ya kumalizika kwa mchezo Samata akafunga goli la tano na kuifanya Genk kuondoka ugenini na hazina kubwa ya magoli  kwani watatakiwa kufungwa 4-0 katika mchezo wa nyumbani wiki ijayo ili kuondolewa katika michuano. Je, watafuzu kwa robo fainali?


No comments:

Post a Comment