TANGAZA NASI HAPA

Thursday, 2 March 2017

LA LIGA: Jovetic akosa ‘tuta’ Sevilla ikishinda dhidi ya Bilbao, Atletico Madrid mambo magumu




GOLI pekee lililofungwa na mshambulizi, Vicente Iborra dakika ya 14’ lilisimama hadi mwisho  wa  mchezo na kuwapa  wenyeji Sevilla  ushindi wa  goli 1-0 dhidi ya Athletic  Bilbao katika pambano  la  ligi kuu Hispania-La Liga usiku wa Alhamis hii katika dimba la Ramon Sanchez Pizjuan.

Mkwaju wa penalty uliopigwa na kiungo-mshambulizi, Steven Jovetic dakika ya 14’ uliokolewa kwa miguu  na  golikipa wa Bilbao, Gorka Iraizoz Moreno lakini Iborra aliuwahi mpira huo uliokolewa na kupiga kiki ya karibu iliyompita kwenye kwapa kipa huyo wa Bilbao  na kuiandikia Sevilla goli hilo pekee.  

Vijana hao wa kocha Muargentina, Jorge Sampaoli wameendelea kuwabana vigogo FC Barcelona na Real Madrid katika  mbio  za ubingwa baada ya kufikisha pointi 55 ( alama mbili nyuma ya vinara Barcelona na pointi moja nyuma ya Real)
 Katika mchezo mwingine uliopigwa Alhamis hii, Atletico Madrid bado wameendelea  kuwa na  msimu mgumu katika La Liga baada ya kulazimika kusawazisha goli la dakika ya 13’ la Florin Andone na kuambulia sare ya kufungana 1-1 dhidi ya Deportivo La Coruna katika dimba la Riazor. 

Mshambulizi wa Ufaransa, Antoine Griezmann alifunga goli la kusawazisha dakika ya 68’. Kufuatia sare hiyo Atletico wamesalia nafasi ya nne katika  msimamo wakiwa na pointi 46 baada ya kucheza michezo 25 huku wakifuatwa kwa karibu na Real Sociedad ambao wana  alama 45.

LIGI hiyo itaendelea leo Ijumaa kwa mchezo  mmoja  utakaozikutanisha  timu za Real Betis na Sociedad.

No comments:

Post a Comment