TANGAZA NASI HAPA

Thursday, 2 March 2017

Baada ya kuangukia kichwa, Fernando Torres anaendelea vizuri Hospitali




 Mshambuli RAIA WA Hispania, Fernando Torres anaendelea vizuri baada ya kuanguka na kuumia kichwa wakati wa mchezo wa ligi kuu ya Hispania kati ya Deportivo La Coruna na AtleticoMadrid. Kwa mujibu wa ripoti ya daktari mshambulizi huyo wa zamani wa Liverpool, Chelsea na Ac Milan hajapata matatizo yoyote  ndani ya kichwa.
Torres alianguka vibaya na kufikia kichwa baada ya kuruka juu kuwania mpira dakika ya 85’ katika tukio ambalo lilizua hofu kubwa katika uwanja wa Riazor. Huduma nzuri ya kwanza aliyopata kutoka kwa madaktari uwanjani hapondiyo ilisaidia kuokoa maisha ya mshambulizi huyo.
 Kupitia mtandao wa klabu ya Atletico Madrid umeripoti kuwa Torres anaendelea vizuri hospitali na anataraji kurejea uwanjani haraka.

No comments:

Post a Comment