Na Baraka Mbolembole
LICHA ya kuangusha pointi tano katika michezo mitatu
iliyopita ya ligi kuu ya kandanda Tanzania bara, mabingwa watetezi wa ligi hiyo
ni michuano ya FA Cup, timu ya Yanga SC bado inaamini inaweza kushinda wa
ubingwa huo kwa mara ya tatu mfululizo msimu huu.
Kikosi hicho kilichokusanya pointi 53 katika michezo 24
ya VPL kinataraji kuwavaa Kiluvya United ya Pwani katika mchezo wa hatua ya 16
bora katika TFF Confederation Cup 2016/17.
" Bado tutaendelea kukosa huduma za baadhi ya
wachezaji wetu katika mchezo wa Jumanne hii dhidi ya Kiluvya kutokana na
majeraha waliyonayo. Hatuwezi kuanza kufikiria mchezo wa Zanaco wakati
tunakabiliwa na mchezo mwingine muhimu katika michuano ya FA." anasema
kocha msaidizi wa Yanga, Juma Mwambusi.
Yanga ilipoteza
2-1 dhidi ya Simba kisha wakashinda 2-0 mbele ya Ruvu Shooting, Jumapili iliyopita
wakalazimisha suluhu-tasa dhidi ya Mtibwa Sugar katika uwanja wa Jamhuri,
Morogoro.
" Vijana walipambana katika mchezo uliopita dhidi ya
Mtibwa lakini tukakosa bahati kidogo na kupata matokeo tuliyopata ya pointi
moja, matokeo hayo hayatoshi kusema sisi tumetoka katika mbio za ubingwa, lakini
vilevile nawaomba mashabiki wetu wazidi kutuunga mkono. Waje kwa wingi katika
mchezo wetu wa leo ili kuwapa motisha vijana, kuwahamasisha ili tuweze kufanya
vizuri zaidi katika mchezo ambao ni 'wa mtoano,' ukishinda unaendelea,
ukishindwa una nje ya michuano."
No comments:
Post a Comment