MABINGWA watetezi wa ligi kuu ya soka Tanzania bara, timu ya
Yanga SC inataraji kuondoka jijini Dar es Salaam mapema asubuhi ya Jumamosi kuelekea mkoani
Morogoro ambako watacheza na Mtibwa Sugar FC katika uwanja wa Jamhuri,
Morogoro.
Katibu mkuu wa klabu hiyo, Charles Boniface Mkwassa
amethibisha hilo. Yanga itacheza na Mtibwa katika mchezo wa 24 msimu huu, hadi
sasa wapo nafasi ya pili nyuma ya Simba kwa tofauti ya pointi mbili baada ya
kukusanya alama 52 katika michezo 23 waliyokwishacheza.
"Kesho pia watafanya mazoezi pamoja na kuuzoea uwanja wa Jamhuri ambao utatumika siku ya mchezo (jumapili) dhidi ya Mtibwa, kama utawala tutahakikisha kila kitu kinaenda sawa ni pamoja na kuaandaa fungu la fedha kulipia gharama zote mkoani humo ili kuepuka kuingia madeni."
No comments:
Post a Comment