TANGAZA NASI HAPA

Wednesday, 8 March 2017

Daktari Yanga SC: Ngoma,Tambwe, Kamusoko wako tayari kuivaa Zanaco, isipokuwa….



 

 WAKATI wapinzani wao Zanaco FC kutoka Zambia wakitaraji kuingia nchi saa kumi jioni leo Alhamis wachezaji Donald Ngoma, Amis Tambwe, Juma Abdul,Thaban Kamusoko wote wameanza mazoezi kujiandaa na mchezo wa Jumamosi hii katika Caf Champions league.

Awali wachezaji hao walizua hofu ya kuukosa mchezohuo wa kwanza hatua ya mwisho kabla ya kufuzu kwa hatua ya makundi kutokana na majeraha yaliyokuwa yakiwakabili. Daktari wa Yanga SC,  Dk. Babu amethibisha kuwa wachezaji hao wanaweza kucheza mchezo huo isipokuwa mlinda mlango Beno Kakolanya na beki Pato Ngonyani pekee.

  Wachezaji wote waliokuwa na majeraha wameshaanza mazoezi Jumatano hii,isipokuwa wachezaji wawili Beno Kakolanya na Pato Ngonyani ambaye alikuwa na maralia na wanaendelea na matibabu lakini wengine wote wameshaanza mazoezi. Mashabiki wa Yanga waondoe wasiwasi kwa sababu Tambwe,Ngoma na Kamusoko wote wapo vizuri na wanaweza kutumika katika mchezo wa Jumamosi ikiwa watapewa nafasi na benchi la ufunzi.” Anasema Dk. Babu

No comments:

Post a Comment