TANGAZA NASI HAPA

Wednesday, 8 March 2017

UEFA CL: Aubematang apiga ‘hat trick’ Dortimund ikifuzu robo fainali…




 Mshambulizi wa Gabon, Pierre-Emerick Aubemayang alifunga magoli matatu ‘hat trick’na kuisaidia Borussia Dortimund kufuzu kwa robo fainali ya michuano ya ligi ya mabingwa ulaya. Kwa jumla ya magoli 4-1 dhidi ya Benfica ya Ureno.

Aubameyang alifunga goli la kwanza dakika ya 4’ akimalizia pasi ya Christian Pulisic.hadi mapumzikio BVB walikuwa mbele kwa goli 1-0. Pulisic akaongeza goli la pili dakika 59’,kabla ya Aubameyang kufunga magolimengine mawili dakika za 61’ na 85’ na kuisaidia timu yake kufuzu kwa robo fainali sambamba na timuza FC Bayern Munich,  Real Madrid na Barcelona.

No comments:

Post a Comment