TANGAZA NASI HAPA

Friday, 3 March 2017

LA LIGA: Sociedad yaipiga Betis na kukwea nafasi ya Nne, Real Madrid ugenini, Barca nyumbani leo




 

MAGOLI ya Jon Bautista 6’, na Xabier Prieto 26’, 72’ yametosha kuwapa ushindi muhimu ugenini Estadio Benito Villamarin timu ya Real Sociedad baada ya kuibuka na ushindi wa magoli 3-2 dhidi ya wenyeji Real Betis katika mchezo wa ligi kuu Hispania-La Liga uliopigwa usiku wa Ijumaa.

Magoli ya Betis yalifungwa na Aissa Mandi 16’, na Antonio Sanabria 65’. Ushindi huo umewapeleka Sociedad hadi nafasi ya nne  katika msimamo wakiwa na alama 48-pointi mbili zaidi ya Atletico Madrid.

Ligi hiyo itaendelea kwa michezo huku vigogo FC Barcelona na Real Madrid pia wakishuka viwanjani. Hii hapa ratiba kamili ya game za leo Jumamosi.

14:00 Leganes ? - ?  Granada

17:15 Eibar ? - ?  Real Madrid

19:30 Villarreal ? - ?  Espanyol

21:45 Barcelona ? - ?  Celta Vigo

No comments:

Post a Comment