Na Baraka Mbolembole
MABINGWA watetezi wa ligi kuu Tanzania Bara,timu ya Yanga SC
imeendelea na mazoezi yake
kujiwinda na mchezo dhidi ya Mtibwa Sugar ambao utapigwa siku
ya Jumapili hii katika uwanja
wa Jamhuri, Morogoro.
Kuelekea mchezo huo mgumu,kikosi hicho kilicho chini ya makocha Mzambia, George Lwandamina na
msaidizi wake Juma
Mwambusi kinakabiliwa na changamoto
kubwa ya majeraha
hasa katika eneo
la ushambuliaji.
Ikiwa tayari
imekata rufaa kupinga
kadi nyekundu aliyooneshwa mshambulizi
wake Obrey Chirwa
katika mchezo wa ushindi
wa 2-0 dhidi ya Ruvu
Shooting Jumatano iliyopita hadi sasa
Yanga haina uhakika
wa kumtumia mshambuliaji
yoyote yule wa
kigeni kati ya
washambuaji watatu
waliofunga jumla ya
magoli 25.
Mzimbabwe, Donald
Ngoma anaendelea kuuguza majeraha
yake ya goti
aliyopata mwezi Januari, Mrundi, Amis Tambwe
alishindwa kufanya mazoezi
siku ya Alhamis
kutokana na maumivu
ya goti, huku suala la
rufaa ya Chirwa
likisubiriwa kutolewa uamuzi
na Shirikisho la
soka nchini TFF kupitia
Bodi ya ligi, huenda
washambuaji wazawa, Emmanuel Martin na Matheo Anthony wakapewa nafasi
katika mchezo huo.
“ Tumeendeleana mazoeizi
Alhamis hii kujiwinda na mchezo
ujao dhidi ya
Mtibwa utaofanyika Morogoro, tunashukuru wachezaji wako katika
hali nzuri, majeruhi ni wachache, kuna Juma
Abdul ambayeambaye anasumbuliwa
na kifundo cha mguu, Donald Ngoma kama mnavyojua
bado hajapona.”
“ Amis Tambwe hatuji
kama anaweza kucheza katika mechi inayokuja. Tambwe ana tatizo katika goti na alianza kusikia
maumivu mara baada ya kumalizika kwa mchezo dhidi ya
Ruvu na Leo ( Alhamis) ameshindwa kufanya mazoezi
vizuri hivyo tunategemea ripoti
maalumu kutoka kwa daktari ili kujua hali
yake.” Anasema kocha
msaidizi wa kikosi
hicho Juma Mwambusi
No comments:
Post a Comment