Na Baraka Mbolembole
BAADA ya kupokea
kipigo cha 2-1 kutoka
kwa mahasimu wao Simba
SC siku ya
Jumamosi iliyopita,mabingwa watetezi
wa ligi kuu
Tanzania Bara, timu ya
Yanga SC Leo Jumatano
itashuka uwanja wa
Taifa Dar es
Salaam kuwavaa Maafande wa
Ruvu Shooting katika muendelezo wa
michezo ya ligi
kuu.
Yanga ilikuwa ikijifua
tangu Jumatatu lakini
kwa mara nyingine wataingiza
timu yao uwanjani
bila huduma ya
mshambulizi Mzimbabwe,
Donald Ngoma ambaye
bado anasumbuliwa na matatizo ya goti.
Ikiwa na pointi 49
baada ya kucheza
michezo 22 kikosi hicho cha
kocha Mzambia, George Lwandamina
kitalazimika kushinda ili kupunguza
‘gepu’ la pointi
tano dhidi ya vinara
Simba ambao tayari
wamecheza michezo 23.
Yanga imeingia katika
kipindi kingine kigumu
msimu huu baada ya kupoteza mchezo
wa tatu Jumamosi
iliyopita. Mara baada ya
kucheza na Shooting
timu hiyo itasafiri hadi
mkoani Morogoro kuwavaa Mtyibwa
Sugar katika uwanja
wa Jamhuri sehemu ambayo
wamefanikiwa kushinda mara
moja tu katika
miaka nane iliyopita.
“ Timu imejiandaa
vizuri, naweza kusema maandalizi kuelekea
mchezo wa Jumatano
hii yameshakamilika. Timu ilikuwa
ikifanya mazoezi tangu
siku ya Jumatatu, jana pia walifanya
mazoezi ya jioni sasa
wako kambini tunasubiri jioni
waingie uwanjani kucheza mechi.”
Anasema Mkwassa mchezaji na
kocha wa zamani
wa klabu hiyo.
“ Sisi kama uongozi
tunajua tunakwenda kucheza
mechi nyingine ngumu, vijana itabidi
wajipange vizuri ili kuweza
kupata matokeo mazuri. Kama unavyojua
mechi iliyopita hatukupata
matokeo mazuri kwa hiyo
ili kuwaamsha tena
mashabiki wetu tunahitaji kupata
matokeo mazuri ili kurudisha moto
tuliokuwa nao. Jukumu kubwa ni
la wachezaji pamoja na
benchi la ufundi kuweza
kuamsha hiyo morali
na sisi kama
uongozi tuko nyuma
yao.”
“ Kuhusu Donald Ngoma
ni kwamba taarifa
nilizokuwa nazo ni kwamba bado
anasumbuliwa na majeraha hivyo hatoweza
kutumika katika mchezo
wa Leo.”
No comments:
Post a Comment