TANGAZA NASI HAPA

Sunday, 26 February 2017

AS Roma yaipiga Inter Milan Giusseppe Meazza na kuendelea kuifukuza Juventus




 IKICHEZA  nyumbani, Geusseppe  Meazza, timu  ya  Inter  Milan  ilikubali  kipigo  cha  mabao  3-1  kutoka  kwa  AS  Roma  katika  mchezo  wa  ligi  kuu  ya  Italia  Serie A. Kiungo, Radja Nainggolan alifunga  mara  mbili  katika  dakika  za 12’ na 56’ kabla  ya  nahodha  wa  Inter, Mauro  Icardi kufunga  goli  la  kufutia  machozi  dakika  ya 81’.

 Diego Perotti aliifungia  Roma  goli  la  tatu  kwa  mkwaju  wa  penalty  zikiwa  zimesalia  dakika  tano mchezo  kumalizika  na  kuendelea  kuwafukuza  mabingwa  mara  nne mfululizo Juventus  ambao  waliibuka  na  ushindi wa 2-0  siku  ya Jumamosi  dhidi  ya  Empoli. Juventus  wanaongoza  ligi  kwa  tofauti  ya  pointi Saba huku  zikiwa  zimesalia  mechi  kumi  kabla  ya kumalizika kwa msimu

 Juve  wamekusanya  alama  66, Roma wana pointi  59 huku  SS Napoli  ambao  walichapwa 2-0   nyumbani  na Atalanta  wanashika  nasfasi  ya tatu  wakiwa  na  alama  54. Ligi  hiyo  itaendelea tena  usiku  wa  Jumatatu  hii  kwa  Fiorentina  kuwakaribisha  Torino.


HAYA HAPA  MATOKEO  YOTE  YA  SERIE A  MZUNGUKO  WA  26

February 25

FT SSC Napoli 0 - 2  Atalanta

FT Juventus 2 - 0  Empoli

February 26

FT Palermo 1 - 1  Sampdoria

FT ChievoVerona 2 - 0  Pescara

FT Crotone 1 - 2  Cagliari

FT Genoa 1 - 1  Bologna

FT Lazio 1 - 0  Udinese

FT Sassuolo 0 - 1  AC Milan

FT Inter 1 - 3  Roma

February 27

21:45 Fiorentina ? - ?  Torino




No comments:

Post a Comment