SHIRIKISHO la Soka
nchini-TFF limeufungulia uwanja
wa Jamhuri,Morogoro kwa
matumizi yamichezo ya
ligi kuu Tanzania
Bara msimu unaoendelea.
Uwanja huo
ulifungiwa kwa muda
usiojulikana mapema mwezi Januari
mara baada ya
mchezo wa ligi kuu
kati ya wenyeji
Mtibwa Sugar dhidi
ya Simba SC kutokana
na ubovu wa
eneo la kuchezea-pitch.
TFF iliufungia Uwanja wa Jamhuri ili kutoa fursa kwa
wamiliki wake kuufanya marekebisho makubwa kwenye eneo la kuchezea huku askari
polisi kupata maelekezo ya kutosha ya jinsi ya kusimamia usalama uwanjani
badala ya kutazama mechi.
Kwa maana hiyo
mchezo wa Machi 5
kati ya Mtibwa
na mabingwa watetezi Yanga
SC utachezwa katika uwanja
huo uliopo katikati ya
mji wa Morogoro baada ya Chama cha
Soka Manispaa ya
Morogoro na wamiliki
wa uwanja huo kufanya
jitihada kubwa kurekebisha
mapungufu yaliyokuwepo awali.
PICHA kwa hisani ya Dastan Shekidele
No comments:
Post a Comment