TANGAZA NASI HAPA

Sunday, 26 February 2017

Paris yaifanyia ‘mauaji’ Marseille, Depay mambo safi Lyon





 IKICHEZA nyumbani Stade Orange Velodrome, timu ya Olympique  Marseille  ilikubali  kipigo  ‘kizito’  kutoka  kwa  PSG. Mlinzi wa  kati, Mbrazil, Marquinhos alifungua ‘karamu’  ya  magoli  dakika  ya 6’,  kisha Edson Cavanni  dakika  kumi baadae akafunga  goli  lake  la  26  katika Ligue 1 msimu  huu.

Mabingwa  hao  watetezi walikwenda  mapumziki  wakiwa  mbele  kwa  magoli 2-0. Lucas  Moura  alifunga  goli  la  tatu dakika  ya 50’, Mjerumani, Julian Draxler akaongeza  linguine  dakika  ya 61’  na  kufanya  matokeo  kuwa  4-0.

Rod Fanni aliwafungia  wenyeji  goli  la  kufutia  machozi  dakika  ya  70’, dakika  tatu  baadae  kiungo Blaise Matuidi akafunga  goli  la  tanoupande  wa  PSG  na  hivyo  kondoka  na  ushindi  huo  mnono  unaowafanya  kuendelea  kuwafukuza  AS  Monaco walio  kileleni  na  alama 62. PSG  imefikisha  pointi 59  huku zikiwa zimesalia  mechi  tisa  kabla  ya  kumalizika  kwa  msimu.



DEPAY  APIGA  MBILI  LYON  IKIUA  5-0
 Kiungo mshambuliaji  aliyeshindwa  kutamba  Manchester  United,Mholland, Memphis Depay ameendelea  kufurahia  uhamisho  wake  wa kujiunga  na  Olympic  Lyon ya  Ufaransa  mwezi  Januari. Depay  alifanikiwa  kufunga magoli  mawili  katika  ushindi  wa 5-0  dhidi  ya Metz.

Alifunga  dakika  za  43’, 53’,  na  kumtengenezea  goli Alexandre Lacazette dakika  ya  78’. Magoli  mengine  ya  mabingwa  hao  mara  saba  mfululizo  wa  zamani  yalifungwa  na Ivan Balliu ambaye  alijifunga  dakika  ya  74 na Mathieu Valbuena aliyefunga  dakika  ya  mwisho  kabisa  ya  mchezo.




MATOKEO  YOTE  YA  LIGUE 1 WIKENDI  JANA HAYA HAPA
February 24

FT Nantes 3 - 1  Dijon

FT Nice 2 - 1  Montpellier

February 25

FT Guingamp 1 - 2  Monaco

FT Angers 3 - 0  SC Bastia

FT Lille 2 - 3  Bordeaux

FT Nancy 0 - 0  Toulouse

FT Rennes 1 - 0  Lorient

February 26

FT Saint-Etienne 0 - 1  Caen

FT Lyon 5 - 0  Metz

FT Marseille 1 - 5  Paris Saint Germain

No comments:

Post a Comment