BRIGHTON& Hove Albion itaikaribisha
Newcaste United katika
dimba la The American Express
Community usiku wa Leo
katika mchezo muhimu
wa ligi daraja
la kwanza England ‘Championship’.
Timu hizo mbili zimekuwa na msimu mzuri
katika Championship na
mara kwa mara zimekuwa zikiteremshana kileleni. Brighton & Hove Albion
inaongoza msimamo hadi
sasa ikiwa na
alama 71 baada ya
kucheza michezo 33 huku Newcastle
ikifuatia ikiwa na
pointi 70 baada ya
kushuka dimbani mara 33 pia.
Mchezo wao wa
kwanza msimu huu Mwezi
Agosti, 2016 kikosi cha
kocha RafaeL Benitez
kilifanikiwa kuchomoza na ushindi
wa magoli 2-0 katika
uwanja wa St.James Park,
shukrani kwa magoli
ya Jamaal Lescells 15’, na
Jonjo Shelvey 63’ lakini tangu
wakati huo kikosi
cha Chris Hughton
kimeimarika na sasa kinawania nafasi ya kupanda ligi kuu msimu ujao
kama mabingwa.
Timu hizo zimekutana mara tatu na
mara mbili ambazo ‘Toon’
wamekwenda The American Express
hawajawahi kushinda. Januari 28, 2012 Brighton iliichapa
Newcastle 1-0 na kuwaondoa
katika michuano ya
FA Cup, Januari 5, 2013 Newcastle
ililala tena 2-0 na kuondolewa katika
michuano ya FA.
Kocha wa Brighton, Hughton aliwahi
kuisimamia Newcastle na
kuipandisha ligi kuu
msimu wa 2009/10
na sasa anaweza
kufanya hivyo kwa
mara nyingine akiwa
na kikosi hicho
cha Brighton msimu huu.
Mshambulizi mwenye miaka
27, Dwight Gayle amefunga
magoli 20 katika
michezo 24 aliyoichezea
Newcastle katika Championship na ndiye kinara wa
magoli katika ligi
hiyo.
Glenn Murray ‘babu’ mwenye
umri wa miaka 33
amekuwa mfungaji kiongozi
wa Brighton msimu huu akifunga
magoli 16 katika
michezo 33. Nani ataibeba
timu yake Leo? Tusubiri na kuona.
MECHI ZA LEO
JUMANNE KATIKA CHAMPIONSHIP
21:45 Aston Villa ? - ? Bristol City
21:45 Blackburn Rovers ? - ? Derby
County
21:45 Brighton & Hove Albion ? -
? Newcastle United
No comments:
Post a Comment