TANGAZA NASI HAPA

Tuesday, 28 February 2017

LA LIGA; Valencia yashinda, Betis yaipiga Malaga, Barcelona, Real Madrid uwanjani Leo




REAL Sociedad ililazimishwa  sare  ya  kufungana 2-2 nyumbani Estadio  Anoeta  dhidi  ya Eibar . Juanmi  aliwafungia  wenyeji  goli  la  kuongoza  dakika  ya  14’. Goli  hilo  lilidumu  kwa dakika  12  tu  baada  ya  Gonzalo Escalante  kuisawazishia  Eibar  dakika  ya 26’.

Mchezo  huo ulikwenda  mapumzik  timu  hizo  zikiwa  sare  ya  kufungana  1-1 na  mara  baada  ya  kuanza  kwa  kipindi  cha  pili,  kadi  mbili  nyekundu  zilitolewa. 

Dakika  ya Florian Lejeune alioneshwa  kadi  ya  pili  ya  manjano  na  kuondolewa  uwanjani  upande  wa  Eibar, dakika  ya  59’, Juanmi  wa  Real  Sociedad  naye  akaondolewa  uwanjani  kwa  kati  ya  pili  ya  njano  iliyoambatana  na  ile  nyekundu.

Mshambulizi wa  Mexico, Carlos  Vela  aliwafungia  Sociedad goli  la  pili  kwa  mkwaju wa  penalty na  huku  ikionekana  kama  wageni  wamelala, dakika  ya  tatu  ya  muda  wa  nyongeza Pedro  Leon akaisawazishia  Eibar.
 Katika  mchezo  mwingine  katika  dimba  la  Mestalla, wenyeji  Valencia  walishida  1-0 dhidi  ya Leganes. Goli  pekee  katika  mchezo  huo  lilifungwa na  mlinzi Eliaquim Mangala dakika  ya  29’. Leganes  ilicheza  pungufu  mchezaji  mmoja  kufuatia  kadi  mbili  za  njano  alizooneshwa Alberto. 
 Ikicheza  ugenini  Estadio La Rosaleda, timu  ya  Real  Betis  ilitoka  nyuma 1-0  na  kuishinda  Malaga  katika  mchezo mwingine  uliopigwa  usiku  wa  Jumanne. Pablo Fornals aliifungia  Malaga  goli  la  uongozi  dakika ya 39’.

Jonas Martin aliisawazishia  Betis  dakika  ya  48’ na  zikiwa  zimesalia  dakika  16 mchezo  kumalizika Antonio Sanabria  akafunga  goli  la  ushindi  na  kuwapa  Betis  ushindi 2-1.

MECHI  ZA  LEO KATIKA  LA  LIGA

FT Real Sociedad 2 - 2  Eibar

FT Malaga 1 - 2  Real Betis

FT Valencia 1 - 0  Leganes

March 1

20:30 Barcelona ? - ?  Sporting Gijon

20:30 Osasuna ? - ?  Villarreal

22:30 Celta Vigo ? - ?  Espanyol

22:30 Granada ? - ?  Alaves

22:30 Real Madrid ? - ?  Las Palmas

No comments:

Post a Comment