Na Baraka Mbolembole
KATIBU Mkuu wa
klabu ya Yanga SC,Charles
Boniface Mkwassa amekiri
klabu yake kudaiwa na mlinzi
wa kimataifa wa Togo, Vicent Bossou.
Mlinzi huyo wa
kati ilidaiwa ni mgonjwa
wa nyonga ndiyo maana hakupangwa katika mchezo
wa kichapo cha 2-1
kutoka kwa Simba SC siku
ya Jumamosi iliyopita, lakini ukweli
mchezaji huyo wa
timu ya Taifa ya
Togo aligomea mchezo
huo kwa madai ya
kudai mishahara yake
ya miezi minne.
“ Nachofahamu
mimi ni kwamba
kuna mishahara ya mwezi
wa nane ambayo ilicheleweshwa, si kwa
Bossou tu ni
timu nzima. Mshahara wa mwezi
wa 12 zikiwa
zimebaki siku kumi kila mchezaji
aliandikiwa cheki, wakalipwa pamoja
na mshahara wa mwezi
wa kwanza.” Anasema Mkwassa
Kupitia kurasa ya
mtandao wake wa kijamii
Bossou aliweka wazi
kuwa hajalipwa mshahara wa miezi
minne sasa na
kuutaka uongozi wake kumlipa
haraka.
“ Sasa wakati
cheki zinatoka, Bossou alikuwa
alikuwa kwenye mashindano AFCON kule Gabon na
yule mtoa cheki hakumkabidhi mtu
yeyote cheki ya
mtu mwingine hadi
muhusika mwenyewe awepo kwa hiyo cheki
ya Bossou ilirudi
ofisini. “
“ Alivyorejea tulimwambia
afuatilie cheki yake lakini
hakwenda na tumejaribu kufuatilia
tumeona kuna matatizo kidogo. Mshahara wa
mwezi wa pili
kila mchezaji bado hajapokea
kama unavyojua timu
yetu ina matatizo kidogo kwa
mwenyekiti hivyo mambo mengi yamesimama.”
No comments:
Post a Comment