Na Baraka Mbolembole
KOSA
la kwanza la kocha, George Lwandamina ni kumuacha benchi nahodha, Nadir Haroub
na kumuanzisha Vicent Andrew katika nafasi ya beki wa kati.
Kocha
wa Simba, Joseph Omog hasingeweza kuepuka kumpanga Novatus Lufunga kama
mlinzi-pacha wa Abdi Banda kutokana na majeraha ya Mzimbabwe, Method Mwajale.
Kabla
ya mechi niliandika katika 'Jicho la 3' kwamba, Simba hawapaswi kuwaanzisha
washambuliaji wake watatu, Laudit Mavugo, Juma Liuzio na Ibrahim Ajib. Pia
nilisema ili 'kujaribu' kuifunga Yanga, Omog anapaswa kuwapanga James Kotei,
Said Ndemla, Muzamiru Yassin na Mohamed Ibrahim.
PENALTI DAKIKA YA 3'
Mzambia, Obrey Chirwa alilazimisha
kumpita mlinzi wa kati wa Simba, Lufunga. Akitambua fika yupo ndani ya eneo la
hatari huku Lufunga akiwa nyuma yake, Chirwa alikimbia 'kikakamavu' lakini
'alilegea' na kuanguka baada ya mguu wa kushoto wa Lufunga kumgonga kwa nyuma
katika mguu wake wa kushoto. Ilikuwa penalti dhahiri iliyoambatana na kadi ya
njano kwa mlinzi huyo wa Simba.
MABADILIKO YA KWANZA-KUMTOA LIUZIO NA
KUMPA NAFASI NDEMLA DAKIKA YA 26'
Kitendo cha kuwapanga kwa wakati mmoja
Mavugo, Liuzio na Ajib ndiyo kulifungua nafasi ya Justine Zulu, Thaban Kamusoko,
Haruna Niyonzima na Msuva kutawala kiungo cha Simba. Nilisema awali kuwa
washambuliaji hao watatu wa Simba huwa hawana msaada mkubwa kiukabaji.
washambuliaji hao watatu wa Simba huwa hawana msaada mkubwa kiukabaji.
Zulu alikuwa akikaba na 'kuua' njia
zote za viungo wa Simba kupeleka pasi kwa washambuliaji wao. Kamusoko aliichezesha
timu kwa kasi huku pia akiwa makini katika ukabaji, ili kuwarudisha mchezoni
wachezaji wake ambao waliopotezwa na mkwaju wa mapema wa penalti, kocha Omog
alichukua uamuzi sahihi ambao alipaswa kuufanya kabla ya kuanza kwa mchezo.
Kitendo cha kocha huyo kumtoa Liuzio na
kumpa nafasi Ndemla dakika ya 26' kilimpa faida kama kocha kwa kufanya
mabadiliko yaliyokuwa na faida. Ndemla ni kiungo mwenye uwezo wa kupiga pasi za
umbali mrefu na kuwafikia walengwa.
umbali mrefu na kuwafikia walengwa.
Baada ya kuingia kwa Ndemla, Simba
ikabadilika kiuchezaji. Walipata nyongeza ya pasi ndefu zilizofika. Kotei,
Muzamiru na Mohamed Ibrahim wote si wazuri katika pasi ndefu ndiyo maana
walisumbuliwa sana na viungo wa Yanga kwa sababu ya uchezaji wao wa pasi
fupifupi.
KUUMIA KWA THABAN KAMUSOKO DAKIKA YA 45'
Awali raia huyo wa Zimbabwe alionekana kuwa na siku njema.
Lakini mambo yakaja kubadilika mara
baada ya kuingia uwanjani Ndemla ambaye aliituliza safu ya kiungo ya Yanga
kutokana na mchezo wake wa kupiga pasi ndefu ambazo ziliwafanya hata wachezaji
wa Yanga kuanza 'kukimbizwa.'
Kamusoko alijikuta akitumia nguvu nyingi zaidi na jambo hilo
likapelekea kujitonesha maumivu yake ya goti.
Japokuwa alijikaza na kuendelea kucheza kwa dakika tano
lakini kadri Simba walivyoongeza kasi katika uchezaji wao, Thaban akalazimika
pia kuongeza spidi na matumizi ya nguvu jambo ambalo lilimuongezea maumivu
zaidi. Dakika 15 za mwisho kuelekea muda wa mapumziko Simba walitawala mchezo.
KAMARI ILIYOZAA HASARA NA FAIDA KWA SIMBA
Dakika 6 baada ya kuanza kwa kipindi cha pili, kocha wa
Simba, Omog aliamua 'kucheza kamari.'
Alimpumzisha mlinzi wa kati, Lufunga na kumpa nafasi kiungo mshambuliaji wa
pembeni, Shiza Kichuya. Nadhani Omog alifanya hivyo ili kuilinda timu yake
isicheze pungufu kwa kuhofu huenda Lufunga
angepata kadi nyekundu.
angepata kadi nyekundu.
Mlinzi wa kulia, Mcongoman Besala Bokungu akaenda kucheza
beki ya kati sambamba na Banda, Muzamiru akarudishwa chini zaidi katika beki
namba mbili na kwa vile katikati ya uwanja walikuwepo Mohamed Ibrahim, Ndemla
na Kotei, kocha huyo hakuona hatari yoyote kumpa nafasi Kichuya kwa sababu
upande wa kushoto wa Yanga haukuwa na madhara.
Dakika nne baada ya Bokungu kuhamia nafasi ya beki wa kati
akalambwa kadi nyekundu kwa kosa la kumchezea vibaya Chirwa ambaye alishamuacha
mlinzi huyo wa Simba na bila kuchezewa faulo bila shaka angeenda kufunga. Kile
ambacho Omog alikihofia kumtokea Lufunga kikamtokea Bokungu na kuwaacha
wakibaki pungufu huku wakiwa nyuma 1-0.
ALICHOPASWA KUFANYA LWANDAMINA BAADA YA SUB YA LUFUNGA
Simba walimtoa beki na kumuingiza kiungo mshambuliaji, lengo
lao lilikuwa ni kuongeza nguvu katika mashambulizi. Kama kocha huku pia timu
yake ikiwa mbele, Omog alipaswa kumpa nafasi Geofrey Mwashuiya ambaye ni wing
mzuri mwenye mbinu, kasi na uwezo wa kumiliki mpira.
Kwa kutambua kuwa Muzamiru ni mchezaji wa kiungo, Mwashuiya
angeweza kumsumbua sana na
pengine kumfanya hadi Kichuya arudi nyuma kumsaidia beki wake namba mbili.
pengine kumfanya hadi Kichuya arudi nyuma kumsaidia beki wake namba mbili.
Lakini wala kocha huyo raia wa Zambia hakuwa na habari.
Kuondolewa uwanjani kwa Bokungu huku Simba wakiwa hawana mchezaji mwingine wa
nafasi ya beki, Lwandamina alipaswa kumpa nafasi Emmanuel Martin na mambo
yangekuwa vizuri upande wao.
Baada ya kushindwa
kupanga timu yake vizuri,
Lwandamina alishindwa pia
hata katika ufanyaji wa
mabadiliko na yale
aliyoyafanya hayakukidhi ubora wa
mechi na alifanya katika
muda mbaya.
KOTEI, NDEMLA, KICHUYA ‘NAWAPA TANO’
Mara baada ya
kuondolewa uwanjani kwa
Bokungu, Mghana,Kotei
alienda kucheza katika
beki yakati
sambamba na Banda. Uchezaji wake
ulikuwa zaidi ya
beki, alizuia na
kuipeleka timu mbele kwa kasi kasha
alirudi haraka katika
eneo lake la
ulinzi. Na alipogundua nguvu
ndogo ya Yanga katika mashambulizi akaamua kucheza
kama namba 6. Huyu
ni mchezaji wa ukweli.
Ndemla
aliendelea kuthibisha kuhusu
ninachokisema mara kwa
mara kuwa huyu ndiye
kiungo bora zaidi Mtanzania
kwa wale wachezesha
timu. Alipiga pasi zilizofika,
alikaba na kuichezesha
timu.
Nilipenda pia moyo
wa kipiganaji wa Kichuya
ambaye aliamua kuutafuta
mpira kila mahali,
kusaidia kukaba . pasi yake
ilizaa goli la
kusawazisha na baadae akafunga
goli la ushindi
zikiwa zimesalia dakika 9
mchezo kumalizika.
Kutoka nyuma 1-0
huku wakiwa pungufu
kuanzia dakika ya 55’ na
kushinda 2-1 dhidi
ya Yanga, sawa kuna
vikosi vya Simba
vilishafanya hivyo dhidi ya
Yanga lakini ushindi
huu wa juzi,
niliona jitihada kubwa
za wachezaji , benchi
la ufundi, Simba walitumia
‘udhaifu’ na uwezo
mdogo wa kocha
Lwandamina katika usomaji
wa mchezaji na
wakashinda kwa haki.
No comments:
Post a Comment