Na Baraka Mbolembole
WACHEZAJI wa
zamani na sasa
wameungana kutetea kiwango
cha baadhi ya wachezaji
wa Yanga SC
dhidi ya mahasimu
wao Simba SC
siku ya Jumamosi
iliyopita. Upande wangu sikuvutiwa
na kiwango cha
mlinzi wa kulia
wa Yanga, Juma Abdul
kwa kuzingatia uwezo
wake wa msimu
uliopita na jinsi anavyocheza
sasa.
“ Mimi nina
imani na Juma Abdul kwasababu
ameshapevuka kimpira, changamoto
na mambo ya
soka anayajua vizuri hivyo suala la
kurudisha uwezo wake wa
awali lipo ndani ya uwezo
wake, tumpe muda na siyo kumuhukumu.”
Anasema nahodha wa
Polisi Moro FC, Nahoda
Bakari.
“ Kisa mechi ya Jumamosi ndiyo Juma
alaumiwe? Siku zote mlikuwa
wapi ‘kuwajaji’ . kubalini kufungwa hiyo
ndiyo mechi ya ‘derby’ hata Kessy
angecheza kwa mfano na timu ingefungwa
wangesema kwa sababu
katoka Simba. Tutajaribu kuangalia mbali sio
hapa. Tabu yetu Watanzania
ni kulaumu tu
ndiyo maana soka letu
haliendelei milele.” Anasema mshambulizi
wa zamani wa
Yanga, Jerson Tegete ambaye
sasa anaichezea Mwadui
FC ya Shinyanga.
“ Mchezaji
huwezi kudumu moja kwa
moja katika kiwango, hata ulaya
tunaona wakati mwingine
wachezaji wanashindwa
itakuwa hapa Bongo ambako mnaweza kukaa miezi
mitatu bila kulipwa mshahara. Huyo
Juma
kiwango kimeshuka lini
au juzi baada ya
kufungwa na Simba?” anahoji Tegete
mmoja kati ya
wafungaji bora watatu
wa muda wote
katika ‘Dar-Pacha’
“ Mchezaji ana changamoto kam
umecheza ama unacheza mpira utaelewa. Kwa
hapa Bongo mchezaji anapofanikiwa
kulinda kiwango chake walau
kwa miaka mitano anastahili pongeza hasa kwa
kizazi cha sasa. “
Mchezaji anasafiri kucheza mechi Bukoba mpaka Songea, Mtwara mpaka Mwanza na mshabiki anataka kiwango kilekile wakati viwanja ni vibovu, malipo ‘kiduchu’ huku nyumbani familia ina matatizo. Kila mechi ina falsafa iliyommeza,tujifunze Mpira.” Anasema kipa wa zamani wa timu za Taifa za Tanzania na klabu ya Polisi Morogoro,Madopi Mwingira amuunga mkono Tegete.
“ Ni kweli
kaka Madopi, sema hawajui,ndiyo
maana wanaona watu wakiwa Simba,
Yanga,Manchester United, Real Madrid
hawajui kuwa muda
mwingine kuna mambo yanakuwa
yakiendelea ndani ya klabu. Hatukatai mechi za
Simba na Yanga kuwa zinaleta
mawazo sana kutokana na ushabiki, lakini tubakize maneno ya
akiba siyo kisa timu
yako imefungwa basi utoe
yote.” Anasisitiza Tegete ambaye
ameshafunga magoli matano
katika mipambano ya
Yanga na Simba.
“ Mimi nimecheza
muda mrefu ligi ya
Bongo pamoja na timu
ya Taifa, na sasa
nimeusoma mpira, tujadili
kama ‘wajuzi’. Simba na Yanga
ni kipimo kizuri kwa
mchezaji na timu. Ili mpira uendelee ikiwemo viwango
vya wachezaji, haya ndiyo mambo
muhimu. Moja, ufundi, Pili, waamuzi bora, Tatu, uongozi mathubuti, Nne,
wadau, na Tano matibabu mazuri. Mimi nadhani
namba moja ndiyo
tuangalie, pia makocha,
tujifunze soka.” Anasema Madopi na
kuongeza.
“ Kwa mfano, nimzungumzie Vicent
Andrew ‘Dante’, goli
lililofungwa na Laudit
Mavugo, mjuzi anajua na
ameona beki anaangalia kushoto , mshambuliaji
yupo nyuma anafnga. Kwangu Danteni miongoni
mwa mabeki bora wanaochipukia,
kiufundi mchezaji anatakiwa aangalie mpira, sehemu
iliyowazi na mpinzani
wake. Hapa ndiyo ufundi sasa
unahitajika, kuna principle
of attacks and defence. Mpira ni kuzuia na
kushambulia.”
“ Madopi Mwingira, Jerson Tegete mmetumia vipaji vyenu juu
ya soka kumfahamisha kidogo
mchambuzi Baraka Mbolembole,nashukuru amewaelewa. Uchambuzi wa
mpira wa miguu unahitaji uelewa
wa mpira, uwe mchezaji, uwe
kocha, daktari, meneja, na
waandishi wa habari za
michezo. Umefika wakati tuendane
na wakatisiyo ‘blablaa’ hiyo ni
kazi ya muda
mfupi zaidi duniani, imejaa mizengwe, fitna na
majungu.” Anasema mchezaji nyota
wa zamani wa
Taifa Stars, Athumani Jumapili
Chama.
“uchambuzi wa mpira wa miguu unaitaji uelewa
wa mpira,uwe mchezaji,coach,dk team,meneja team na wahadishi wa michezo hao
wana ueledi,uelewa wa football,imefika wakati tuendane na wakati,sio blablaa
ndo kazi ya muda mfupi zaidi duniani,imejaa mizengwe,fitna,majungu