BARCELONA imepaa
kileleni mwa msimamo wa ligi
kuu Hispania-La Liga baada ya
ushindi wa magoli 6-1 dhidi ya
Sporting Gijon katika uwanja
wa Camp Nou; wapinzani wao Real
Madrid ‘wakikwama’ baada ya
sare ya 3-3 dhidi ya
Las Palmas usiku wa Jumatano hii
katika dimba la Santiago Bernabeu.
Leonel Messi 9’, Luis
Suarez 27’ na Neymar 65’ kila mmoja
alifunga, goli la kujifunga
la Juan Rodriguez 17’, Paco
Alcacer 49’ na Ivan Rakitic 87’ walifunga magolimengine
ya Barca na kuwahakikishia ushindi
mabingwa hao watetezi.
Mwanasoka bora wa
dunia Cristiano Ronaldo
alifunga magoli mawili
ndani ya dakika
tatu za mwisho
na kuinusuru Madrid
kukutana na kipigo
mbele ya Las Palmas katika
mchezo ambao ulishuhudia
staa wa Wales, Gareth
Bale akilambwa kadi
ya pili ya
njano kisshanyekundu dakika ya 47’.
Isco alifunga goli
la kuongoza upande
wa wenyeji dakika ya 8’, lakini goli hilo
lilidumu kwa dakika
mbili tu kabla
ya Pedro Tanausu Dominguez kuisawazishia
La Palmas dakika ya
kumi na hadi
kipindi cha kwanza
kinamalizika timu hizo zilikuwa
sare ya kufungana 1-1.
Jonathan Viera alifunga
goli la pili
kwa njia ya
mkwaju wa penalty dakika
ya 46’ kufuatia
madhambi yaliyofanywa na
nahodha wa Real, Sergio
Ramos. Kevin Prince-Boateng akaongeza
linguine dakika ya 59’ na
kuwafanya wageni kuongoza
3-1.
C.Ronaldo akafunga
kwa mkwaju wa penalty dakika
ya 86’ akaongeza la tatu
dakika 89’ na kuipa sare ya
3-3 timu yake. Kwa matokeo hayo Barcolana imekwea
kileleni ikiwa na alama 57-pointi moja mbele
ya REAL Madrid ambao
wana mchezo mmoja
wa kiporo.
HAYA HAPAMATOKEO
YOTE YA
LA LIGA USIKU WA
JUMATANO
FT Barcelona 6 - 1 Sporting
Gijon
FT Osasuna 1 - 4 Villarreal
FT Celta Vigo 2 - 2 Espanyol
FT Granada 2 - 1 Alaves
FT Real Madrid 3 - 3 Las
Palmas





No comments:
Post a Comment